Alichukua mtoto wangu, alisema, anaenda kumnunulia peremende na biskuti. Ulikuwa uongo.BBC News Swahili2024-10-22 | Alichukua mtoto wangu, alisema, anaenda kumnunulia peremende na biskuti. Ulikuwa uongo.Matangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-13 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwMuziki na soka kwangu mimi ni mchanganyiko mzuri- Kipa bora wa kike AfrikaBBC News Swahili2023-07-13 | Andile Dlamini wa Afrika Kusini ndiye kipa bora wa kike barani Afrika na sasa anajiandaa kwa Kombe la Dunia la FIFA la Wanawake.
Lakini 2021, ilibaki kidogo kuacha mpira baada ya kupata maambukizi ya Covid-19.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 30 alizungumza na BBC namna alivyokabiliana na hali hiyo na jinsi anavyoweza kujihusisha na muziki na soka kwa wakati mmoja.
#bbcswahili #afrikakusini #sokaNapenda kazi yangu initambulishe kuliko kiki - Phina, Mwanamuziki wa TanzaniaBBC News Swahili2023-07-13 | Akitokea katika familia iliyompinga kufanya muziki, mwanamuziki Saraphina maarufu kama @phina_tz amekuwa akikua kimuziki tangu alipoachia kibao chake kinachopendwa na wengi Afrika Mashariki na kati cha ‘Upo Nyonyo’
Anajivunia utunzi bora wa mashairi na utambulisho wake binafsi wa sauti na madaha jukwaani huku baadhi wakimfananisha na @vanessamdee
@phina_tz alizungumza na mtangazaji Kínára wa BBC @roncliffeodit na kuandaa taarifa hii
🎥: @frankmavura
#bbcswahili #tanzania #nyotawaafrikamashariki‘Tunaendesha maisha yetu tukitegemea Uchumi wa buluu’BBC News Swahili2023-07-13 | Idadi kubwa ya watu wanaoishi katika maeneo ya pwani huchangia kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa dunia, mchango wao ukiwa na thamani ya takriban dola trilioni 1.5 za Kimarekani kwa mwaka, hii ni kwa mujibu wa Umoja wa mataifa.
Katika pwani ya Kenya, baadhi ya vijana wanatumia rasilimali ya bahari ili kujikwamua kiuchumi kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kuvutia watalii kupitia michezo ya baharini.
Mwandishi wa BBC @frankmavura ametuandalia taarifa ifuatayo kutoka Mombasa, nchini Kenya.
#tanzania #kenya #uchumiwabluuMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-12 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwChimbuko la hiki kikundi ni mwanangu alikuwa anapokea KipaimaraBBC News Swahili2023-07-12 | Nchini Tanzania kundi la Watoto lijulikanalo kama @tegeta_kids limejizolea umaarufu mkubwa na kujipatia wafuasi wengi katika mitandao ya kijamii ambapo watoto wa umri kati ya miaka 5 hadi 15 huonesha uwezo wao wa kucheza nyimbo za mahadhi mbali mbali.
Mwanzilishi ambaye ni mama muuza maziwa anasema lengo lake ni kufikisha kikundi hiki katika majukwaa ya kimataifa.
Mwandishi wa BBC Veronica Mapunda alikitembelea kikundi hiki kilichopo jijini Dar es Salaama na kuandaa taarifa hii.
#bbcswahili #tanzania #tegetakidsMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-11 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwTunaiambia serikali punda amechoka - Raila OdingaBBC News Swahili2023-07-11 | kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga ameunga mkono msimamo wa mahakama kuhusu Sheria ya Fedha 2023.
Raila Odinga ambaye wiki iliyopita alitangaza awamu nyingine ya maandamano kuanzia jumatano wiki hii, amesisitiza kuwa upinzani hautaahirisha maandamano hayo licha ya uamuzi huo.
#bbcswahili #kenya #railaodingaMjasiriamali wa kutengeneza magitaa TanzaniaBBC News Swahili2023-07-11 | Mjasiriamali mmoja nchini Tanzania, Pardon Modest amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na kipaji alichonacho cha kutengeneza/kuunda magitaa ya umeme kwa kutumia malighafi zinazopatikana nchini humo ikiwemo mbao, nyaya na vipuli mbalimbali.
Sambamba ameweza kutengeneza fursa kwa vijana kwa kuwafundisha stadi hiyo lakini pia jinsi ya kuvitumia.
Mwandishi wa BBC, @lasteck2023 alimtembelea mtaalamu huyo na kuandaa taarifa hii…
#RailaOdinga #GharamaYaMaisha #Maandamano #RoncliffeOdit #Raila #PeterMwangangiWatoto wa Ghana wachukuliwa kwa nguvu kutoka katika makazi yaoBBC News Swahili2023-07-10 | Uchunguzi wa BBC Africa Eye umeibua wasiwasi mkubwa kuhusu mojawapo ya mashirika makubwa duniani ya kupambana na utumwa na operesheni zao za Afrika Magharibi.
Operesheni ya Kimataifa ya Haki (IJM) ilikusanya zaidi ya pauni milioni tatu nchini Uingereza mwaka jana kwa msaada wa kutoka karibu makanisa 300 kote nchini.
Baadhi ya shughuli zinazofadhiliwa na fedha nchini Ghana, IJM inalenga kuwaokoa watoto waliosafirishwa na kuwaunganisha na familia zao.
Hata hivyo, uchunguzi wa siri wa BBC umepata ushahidi kwamba shughuli za shirika hilo la kutoa misaada zimesababisha baadhi ya watoto kuchukuliwa kutoka kwa familia zao, katika msako mkali wa usiku.
#bbcswahili #ghana #afrcaeyeWanaume wa Uganda wafundishwa kufanya kazi za nyumbani.BBC News Swahili2023-07-09 | Shirika moja lisilo la kiserikali nchini Uganda limeanizisha mradi wa kuhamasisha wanaume kufanya kazi za ndani majumbani.
Wana amini kwamba kuwafundisha kupika, kusafisha, kuchota maji na kutunza watoto kutapunguza mzigo kwa wanawake.
#bbcswahili #uganda #wanaumeTuna hasira kwasababu kilichotokea sio sawaBBC News Swahili2023-07-08 | Familia ya Nahel M, mvulana mwenye umri wa miaka 17 aliyeuawa na afisa wa polisi, imeambia BBC haiamini kama ghasia zilizoonekana kote Ufaransa katika siku za hivi karibuni zitaleta haki ya kifo chake.
Nahel M alipigwa risasi moja kwa moja na polisi baada ya kushindwa kusimama ili kukaguliwa na askari wa barabarani Jumanne iliyopita.
"Hatujaitisha ghasia bali matembezi ya amani kwa ajili ya Nahel M," ndugu huyo ambaye jina lake halikujulikana aliambia BBC.
#bbcswahili #ufaransa #parisMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-07 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwMtanzania mwenye asili ya Uingereza anavyopigania lugha ya KiswahiliBBC News Swahili2023-07-07 | Mwandishi wa vitabu na mtunzi wa mashairi Richard Mabala ameiambia BBC ni lazima kukubali kuwa lugha inakua hivyo maneno mapya yanazaliwa kutokana na namna vijana wanavyowasiliana sasa hayana budi kurasimishwa
Mabala ambaye kwa asili ni rai awa Uingereza na sasa ni Mtanzania amekuwa moja ya watu wanaopigania Kiswahili kutumika kama lugha ya kufundishia nchini Tanzania ili kuwezesha wanafunzi kuelewa kwa urahisi
Mwandishi wa BBC @eagansalla_gifted_sounds alizungumza naye na kuandaa taarifa hii
#bbcswahili #kiswahili #sikuyakiswahiliMimi ni msanii wa kwanza kupewa tuzo na RaisBBC News Swahili2023-07-07 | Natacha Ngendabanka ni mmoja wa wasanii maarufu nchini Burundi.
Mbali na kuwa mwanamuziki, Natacha pia ni mfanyabiashara maarufu na balozi wa UNFPA ambaye anahusika na masuala ya kuhamasisha vijana kuhusu uzazi wa mpango.
Mwandishi wa BBC Robert Kiptoo alimtembelea Natacha ambaye ametoa wimbo mpya hivi karibuni na kuandaa taarifa hii.
🎥 @eagansalla_gifted_sounds
#bbcswahili #burundi #muzikiMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-06 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-05 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwRubani mashuhuri anayepigana na Urusi kwa helikopta ya enzi ya UsovietiBBC News Swahili2023-07-05 | Roman 34, ni rubani wa Ukraine ambaye amekuwa akiendesha misheni ya kivita dhidi ya vikosi vya Urusi katika helikopta ya enzi ya Usovieti yenye miaka karibia sawa na umri wake ambayo haina ulinzi wala mfumo wa kisasa wa tahadhari ya makombora
Ameongea na BBC na kuelezea namna anavyokabiliana na hatari ya mashambulizi katika vita hivyo.
#bbcswahili #ukraine #urusiJe unaujua mchezo huu wa kuchapana makofi usoni?BBC News Swahili2023-07-05 | Slap Kabaddi, mchezo unaotaka kufanana na mieleka unaohusisha kuchapana makofi, unazidi kuwa maarufu huko Punjab, Pakistan.
Kabaddi ni mchezo maarufu huko Asia Kusini. Slap Kabaddi, kwa kawaida huchezwa katika sherehe katika mkoa wa kati-mashariki wa Punjab.
#bbcswahili #pakistan #punjabMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-04 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwWairan wanaopoteza masiaha kwa sumu ya pombe na usiriBBC News Swahili2023-07-04 | Wimbi jipya la unywaji wa pombe yenye sumu nchini Iran linaua watu ambao wanaogopa sana adhabu badala ya kutafuta msaada wa haraka wa matibabu.
Pombe imepigwa marufuku katika nchi hiyo ya Kiislamu (isipokuwa kwa baadhi ya dini ndogo), na watu wanaopatikana wakinywa pombe wanaweza kupata adhabu ya viboko 80, kifungo au hata kifo kwa wakosaji wa kurudia.
#bbcswahili #iran #sheriaShinyanga: Mji unaotumia usafiri wa baiskeli kama daladalaBBC News Swahili2023-07-04 | Je unafahamu kuwa nchini Tanzania kuna mji mkongwe ambao usafiri wake mkuu ni baiskeli?
Kwa muda wa miongo mitano sasa, wakazi wake wameendelea kutegemea zaidi usafiri huo ambao unatambua baisikeli za uchukuzi wa umma kwa jina 'daladala'.
Mwandishi wa BBC @lasteck2023 ametembelea mji huo wa Shinyanga uliopo Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo na kuandaa taarifa hii…
📸Nicholaus Mtenga
#bbcswahili #tanzania #shinyangaMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-07-03 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwNilipata mpenzi, nilipomwambia sioni akapotea ghaflaBBC News Swahili2023-07-03 | Francine Niyonkuru ni mtangazaji wa habari asiyeona mwenye umri wa miaka 23 kutoka Burundi.
Daima alikuwa na ndoto ya kuwa mwandishi wa habari na hatimaye ndoto hiyo imetimia.
Anaelezea changamoto na unyanyapaa ambao amekumbana nao katika kutimiza ndoto yake na Jinsi alivyokabiliana nao hadi kuungwa mkono.
#bbcswahili #burundi #ulemavuBBC News SwahiliBBC News Swahili2023-07-02 | Tazama namna Vanilla, sokwe mwenye umri wa miaka 28, alivyotoka nje kwa mara ya kwanza baada ya kukaa ndani ya kizimba chake kwa miaka yote hiyo.
Ni mmoja wa sokwe walionusurika kutoka Maabara ya New York ya Madawa ya Majaribio na Upasuaji katika wanyama (LEMSIP).
Vanilla na dada yake, Shake, wana makazi mapya katika kisiwa chini ya Save the Chimp huko Fort Pierce, Florida.
#bbcswahili #savethechimp #wanyama #sokweNaweza kukaa hadi siku nne kwenye foleni ya mafutaBBC News Swahili2023-07-01 | Kwa miaka kadhaa sasa nchi ya Burundi imekuwa na uhaba wa mafuta hasa petroli na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi wa taifa hilo.
Burundi imekuwa ikipokea shehena yake ya mafuta kutoka bandari ya Dar es Salaam nchini Tanzania na kwa mujibu wa Rais Evariste Ndaishimiye, uhaba huu umesababishwa na wafanyabiashara wenye malori kukataa kuleta mafuta.
🎥@eagansalla_gifted_sounds
#bbcswahili #burundi #uchumiMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-30 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwMlemavu hana shida yoyote na sisi tunawezaBBC News Swahili2023-06-30 | Hortense Kavuo Maliro, 43, ni mwanamke wa kwanza na anayeishi na ulemavu kutangaza kwamba atawania urais wa DRC katika uchaguzi wa Desemba (12).
🎥 Frank Mavura
#bbcswahili #DRC #uchaguzidrcMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-29 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwNilipoteza mikataba ya kazi baada ya kusema hadharani siko sawa kiakiliBBC News Swahili2023-06-29 | Rosa Ree ni mmoja kati ya wanamuziki wakubwa wa Hip Hop nchini Tanzania. Hata hivyo, licha ya ufanisi kimuziki, Rosa Ree alipitia changamoto ya afya ya akili baada ya kujifungua mtoto wake.
Msanii huyo alikumbana na unyanyapaa baada ya kujitokeza na kusema kwamba hayuko sawa.
Na hata alipoteza kandarasi na mikataba kadhaa.
Lakini ni nini kilichomsukuma kusema hayuko sawa? Rosa Ree amemsimulia changamoto zake Mtangazaji kinara wa BBC RoncliffeOdit
#bbcswahili #tanzania #hiphopMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-28 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwKwasababu ya ubunifu huu, nilishinda tuzo ya Muuguzi Bora DunianiBBC News Swahili2023-06-28 | Muuguzi wa Tanzania Wilson Fungameza, alibuni na kutambulisha Kifaa Kilichoboreshwa kinachosaidia watoto wenye matatizo ya kupumua ambapo tangu kimeanza kutumiwa kimesaidia kupunguza vifo vya watoto wachanga vinavyotokana na matatizo ya kupumua nchini humo.
🎥@eagansalla_gifted_sounds
#bbcswahili #tanzania #muuguziMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-27 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwAtembea kutoka Pakistan hadi Mecca kutimiza ndoto ya HajjBBC News Swahili2023-06-27 | Akiwa amebeba mwavuli na begi lake, mwanafunzi wa Pakistan ametembea zaidi ya kilomita 4,000 kufikia ndoto yake ya kufika Mecca kwa miguu kabla ya Hija ya mwaka huu.
Akianza safari yake ya miezi sita kutoka mji alikozaliwa wa Okara, Usman Arshad alipitia Pakistan, Iran, Umoja wa Falme za Kiarabu na Saudi Arabia na hatimaye kufika mji mtakatifu wa Mecca.
#bbcswahili #mecca #iddelhajjUshahidi wa uwezekano wa uhalifu wa kivita Sudan wazukaBBC News Swahili2023-06-27 | "Wafanyakazi katika hospitali nyingi wameshikiliwa mateka, kama njia ya kuwapatia matibabu wanajeshi wa RSF waliojeruhiwa."
Ni hospitali chache kati ya 88 za Khartoum ambazo bado zipo wazi baada ya wiki tano tu za mapigano.
Kwa kutumia takwimu za satelaiti, ramani na maudhui yaliyotokana na mazungumzo ya madaktari kadhaa, uchunguzi wa BBCNewsArabic na BBCAfricaEye unagundua ushahidi wa kutatanisha wa uwezekano wa uhalifu wa kivita unaotekelezwa kwenye vituo vya afya na wafanyakazi na pande zote mbili zinazopigana.
#bbcswahili #sudan #bbcafricaeyeMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-26 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwWaathiriwa wa mafuriko Burundi wazungumzaBBC News Swahili2023-06-26 | Yamekua ni maisha ya shida kwa Bi Nizigiyimana Shadi muathiriwa wa mafuruko katika mji wa Gatumba nchini Burundi.
Bi Nizigiyimana ni mmoja wa raia wanaoishi katika makazi ya muda baada ya wenzake kuhamishwa katika maeneo salama.
Mafuriko katika eneo hili yamekuwa yakitokea mara kwa mara kutokana na mto Rusizi kuvunja kingo zake na kupanda Kwa viwango vya maji katika Ziwa Tanganyika.
Aliielezea BBC masaibu aliyonayo kutokana na athari za mafuriko hayo.
#bbcswahili #burundi #mafurikoKanisa la karne ya 16 laibuka kutoka chini ya maji baada ya ukameBBC News Swahili2023-06-25 | Mabaki ya Hekalu la Quechula la karne ya 16 yaliyokuwa yamefunikwa na maji yameibuka tena huko Mexico kufuatia ukame na joto kali.
Kanisa hilo lilifunikwa na maji wakati Bwawa la Malpaso lilipojengwa katika miaka ya 1960.
Hapo awali wakati maji yanapungua lilionekana kidogo lakini sasa linaonekana lote kabisa.
#bbcswahili #mabadilikotabianchi #ukameWaafghanistan watekwa nyara na kuteswa kwenye mpakaBBC News Swahili2023-06-25 | Uchunguzi wa BBC umefichua kuwa wahamiaji wa Afghanistan wanatekwa nyara na kuteswa ili watoe pesa kwenye mpaka wa Iran na Uturuki.
Video zinatumwa kuwatia hofu familia zao na kuwataka walipe kiasi kikubwa cha pesa ili kuwaachilia wapendwa wao.
Mwandishi wa BBC Soran Qurbani, ambaye aliwahi kusafirishwa kimagendo hadi Uingereza miaka 12 iliyopita kutoka Iran, ametumia miezi kadhaa kufuatilia simulizi za wakimbizi katika njia hiyo.
#bbcswahili #afghanistan #iranUrusi haihesabu askari waliofariki vitaniBBC News Swahili2023-06-24 | Urusi mara chache huweka taarifa kuhusu kupoteza kwake kijeshi.
Lakini uchunguzi uliofanywa na BBC umebainisha zaidi ya wapiganaji 25,000 wa Urusi wamefariki, ikiwa ni idadi ya juu kuliko takwimu rasmi za Moscow.
#bbcswahili #urusi #ukraineJe unaweza kuvaa gauni la harusi ambalo limeshavaliwa na mtu mwinngine?BBC News Swahili2023-06-24 | Vazi la siku ya harusi ni moja ya vitu muhimu na vya gharama kubwa ambalo huvaliwa kwa siku hiyo au pengine kwa saa chache tu hivyo ili kupunguza gharama wengine hukodisha magauni au kununua ya mtumba.
Lakini katika baadhi ya mila na tamaduni za Kihindi ni vigumu kukodi au kununua kitu ambacho kimevaliwa kutokana na imani kuhusu nguo za mitumba.
Maharusi hawa wanaelezea utamaduni huo na maoni yao
#bbcswahili #india #ndoaMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-23 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwAbiria Titan asimulia kukatika kwa mawasilianoBBC News Swahili2023-06-23 | Abiria wa zamani wa chombo cha Titan aelezea changamoto ya kukatika kwa mawasiliano aliyowahi kukutana nayo mwaka 2022 alipokuwa akienda kuangalia mabaki ya meli ya Titanic chini ya bahari.
Mwigizaji wa Mexico na mtengeneza maudhui wa Youtube Alan Estrada alikuwa kwenye chombo cha Titan mwaka jana kilipopoteza mawasiliano wakiwa kina cha karibu mita 1,000, na kusababisha kutaka kukatisha safari hiyo.
Estrada alirekodi msafara huo na kuliambia shirika la habari la Reuters kuwa baadaye mawasiliano yalirejea na chombo kiliweza kuendelea na safari
#bbcswahili #titanic #titanSimulizi ya Binti wa miaka 19 mkimbizi kutoka Congo alivyotekwa na waasiBBC News Swahili2023-06-23 | Akiwa na miaka 13 Kijiji cha Noella kilivamiwa na kundi la waasi, katika harakati za kukimbia akaishia mikononi kwa waasi hao na kupelekwa katika makazi ya kundi hili eneo la msituni ambapo aliolewa na kiongozi wa waasi.
Alifanikiwa kutoroka, lakini baada ya hapo maisha yake yalikuwaje?
Mwandishi wa BBC Peter Mwangangi alikutana nae na kuandaa taarifa hii
#bbcswahili #kenya #wakimbiziMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-22 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwKijana mpigapicha aliyeacha kazi hiyo na kujitosa katika siasa.BBC News Swahili2023-06-22 | Patrick Mbelle Mwavula, Diwani wa kata ya Bamburi, kaunti ya Mombasa, Kenya anaelezea kwa kina sababu iliyomfanya kubadili taaluma yake na kuingia katika ulimwengu wa siasa akiwa na umri wa miaka 29 tu wakati huo.
Je aliweza vipi kuhimili mikiki mikiki ya siasa licha ya umri wake mdogo huku akiwa hana rasilimali wala uzoefu uzoefu wa kutosha kukabiliana na wakongwe wa siasa.?
#bbcswahili #kenya #vijanaMatangazo ya Dira ya Dunia TVBBC News Swahili2023-06-21 | Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGwNdani ya chombo kilichotoweka chini ya majiBBC News Swahili2023-06-21 | Mwaka 2022, BBC ilirekodi ndani ya chombo hicho cha kampuni ya OceanGate ambacho kimepoteza mawasiliano kikiwa na watu watano chini ya Bahari ya Atlantiki.
Mmoja kati ya watalii waliowahi kupanda chombo hicho akizungumza na BBC, alisema "Wote huwa tunajua kuhusu hatari kabla ya kuingia."
Juhudi za uokoaji zinaendelea ili kupata chombo hicho ambacho kilitoweka baada ya kuingia chini ya bahari ya Atlantiki kupeleka watalii katika eneo la ajali ya meli ya Titanic siku ya Jumapili.